- Rukhsana Noor
- Jul 7, 2020
- 0 min read
ROXYRECIPES
- Rukhsana Noor
- Jul 5, 2020
- 0 min read
- Rukhsana Noor
- Jul 5, 2020
- 1 min read

Mahitaji:
Samaki wawili
Chumvi
Limao au ndimu moja
Kitunguu saumu kilichopondwa nusu kijiko cha chakula
Mafuta ya kupikia
Pilipili manga kijiko kimoja cha chakula
Tangawizi iliyopondwa nusu kijiko cha chakula
Binzari ya mchuzi nusu kijiko cha chakula
Kitunguu maji
Hoho
Carrot
Nyanya
Karanga iliyosagwa kijiko kimoja cha chakula
Jinsi ya kupika:
1) Tengeneza samaki wako osha kisha wawekee ndimu au limao, chumvi na pilipili manga nusu kijiko waache kwa dk 30 kisha wakaange uweke pembeni
2) Weka sufuria jikoni, kisha weka mafuta vijiko vitatu vya chakula yakipata moto weka kitunguu maji na carrot kaanga,vikipata rangi weka kitunguu saumu, pilipili manga iliyobaki,binzari ya mchuzi,tangawizi kisha kaanga, kisha weka nyanya na chumvi kidogo funika acha nyanya iive , nyanya ikiiva weka hoho koroga na uweke karanga weka na maji nusu kikombe changanya kisha funika tena mchuzi uchemke, ukisha chemka ukawa mzito weka samaki wako changanya na uache uchemke dk 2 kisha epua utakuwa tayari.