Bugger Sliders
- Rukhsana Noor
- Jul 22, 2020
- 1 min read
Mahitaji:
Unga wa ngano vikombe vinne (kikombe kimoja cha 250ml)
Maziwa ya maji vikombe viwili ( 500ml)
Siagi vijiko viwili vya chakula (yeyusha)
Siagi vijiko vitatu vya chakula (usiyeyushe)
Amira ya chenga vijiko viwili vya chakula
Sukari kikombe kimoja 250ml
Mafuta ya kula kijiko kimoja cha chakula
Jinsi ya kupika:
1) Pasha maziwa yawe vuguvugu kidogo sana kisha weka siagi uloyeyusha, amira ya chenga na mafuta na sukari kidogo koroga kisha acha iumuke amira
2) Chukuwa unga changanya na sukari yote iliyobaki kisha mimina kidogo kidogo katika mchanganyiko wa maziwa na amira kisha kanda unga wako mpaka uchanganyike vizuri uwe Donge kisha tumia vijiko vya siagi visivyoyeyushwa kuwa unapaka katika donge lako huku unakanda mpaka iishe ukimaliza kukanda paka mafuta donge lako funika kwa masaa mawili liumuke
3) Ukishaumuka kata madonge ya sliders zako pakaa mafuta trey ya kuokea uyapange acha nafasi kati ya donge na donge kisha funika kwa dk 45 yaumuke tena kisha yapakae mafuta juu, kisha oka katika moto wa 150c kwa dk45 baada ya hapo zitakuwa tayari.
Comments