top of page
Search

Sauce ya ukwaju

  • Writer: Rukhsana Noor
    Rukhsana Noor
  • Aug 27, 2020
  • 1 min read

Mahitaji:


Ukwaju kiasi utakachopenda (nimetumia mitano)

Chumvi

Binzari nyembamba ya unga/binzari ya pilau kijiko kimoja cha chai

Pilipili iliyosagwa au kupondwa kijiko cha chai (si lazima)

Kitunguu saumu na tangawizi zilizopondwa kijiko kimoja cha chakula

Mafuta ya kupikia kijiko kimoja cha chakula

Masala ya mchuzi kijiko kimoja cha chakula


Jinsi ya kutengeneza:


1) Osha ukwaju na maji safi kisha weka maji kiasi na uchemshe, kisha uchuje utoe kokwa upate rojo na uweke pembeni rojo yako


2) Chukuwa pan weka jikoni, weka mafuta ya kupikia, kisha weka masala ya mchuzi, kitunguu saumu na tangawizi, binzari nyembamba, pilipili kaanga kwa sekunde 10, kisha mimina rojo ya ukwaju uweke na chumvi na anza kuipika huku unaikoroga mpaka iwe nzito kwa uzito unaotaka wewe kisha epua itakuwa tayari, ni nzuri kula na chips, mishkaki n.k



 
 
 

Recent Posts

See All

Comments


© 2020 by Roxy recipes. All rights reserved

  • ooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooroxyrecipes Instagram Account
bottom of page