NYAMA YA KUKAANGA
- Rukhsana Noor
- Mar 24, 2020
- 1 min read
Updated: Mar 27, 2020
MAHITAJI:
Nyama ya Ng`ombe steki nusu kilo
chumvi
mafuta ya kupikia
tangawizi na kitunguu saumu kilichopondwa vijiko viwili vya chakula
soy sauce vijiko vitatu
vinegar kijiko kimoja
pilipili manga ya unga nusu kijiko
JINSI YA KUPIKA:
1) Osha na katakata nyama na uweke katika bakuli pana
2) Weka vitu vyote kasoro mafuta,katika bakuli lenye nyama na uchanganyaje vizuri ukimaliza ifunike ka muda wa masaa matatu
3) Baada ya masaa matatu weka mafuta katika pan tumia moto mdogo mdogo yakipata moto weka nyama zote funika, acha zijipike kwa moto mdogo kwa dakika 40 kisha zigeuze funika tena acha zijipike tena kwa dk 40 kisha geuza fanya hivyo mpaka nyama zako ziive ziwe za brown kisha zitoe katika mafuta tayari kwa kuliwa na ugali au kitu chochote.
Comments