Pilipili ya kukaanga
- Rukhsana Noor
- Jul 22, 2020
- 1 min read

Mahitaji:
Pilipili ndefu kiasi utakachopenda
Mafuta ya kupikia
Nyanya mbili zilizosagwa
Chumvi
Binzari masala kijiko kimoja cha chakula
Binzari ya njano kijiko kimoja cha chai
Kitunguu saumu kilichopondwa kijiko kimoja cha chai
Maji ya limao au ndimu kijiko cha chakula kimoja
Jinsi ya kupika:
1) Osha pilipili zako kisha ziache zikauke maji
2) Weka sufuria jikoni ya mafuta yakipata moto kiasi (yasiwe ya moto sana viungo vitaungua), weka viungo vyote na vikaange kwa sekunde 5, kisha weka nyanya ipike mpaka iive mafuta yaje juu, kisha weka pilipili zote changanya weka chumvi na maji ya limao funika na ipike mpaka pilipili ziive ziwe laini unaweza ongeza maji kidogo ukiona nyanya zinaganda chini. Zikiiva pilipili epua acha ipoe itakuwa tayari kuliwa.
Comments