top of page
Search

Pilipili ya kukaanga

  • Writer: Rukhsana Noor
    Rukhsana Noor
  • Jul 22, 2020
  • 1 min read


Mahitaji:


Pilipili ndefu kiasi utakachopenda

Mafuta ya kupikia

Nyanya mbili zilizosagwa

Chumvi

Binzari masala kijiko kimoja cha chakula

Binzari ya njano kijiko kimoja cha chai

Kitunguu saumu kilichopondwa kijiko kimoja cha chai

Maji ya limao au ndimu kijiko cha chakula kimoja


Jinsi ya kupika:


1) Osha pilipili zako kisha ziache zikauke maji


2) Weka sufuria jikoni ya mafuta yakipata moto kiasi (yasiwe ya moto sana viungo vitaungua), weka viungo vyote na vikaange kwa sekunde 5, kisha weka nyanya ipike mpaka iive mafuta yaje juu, kisha weka pilipili zote changanya weka chumvi na maji ya limao funika na ipike mpaka pilipili ziive ziwe laini unaweza ongeza maji kidogo ukiona nyanya zinaganda chini. Zikiiva pilipili epua acha ipoe itakuwa tayari kuliwa.

 
 
 

Recent Posts

See All

Comments


© 2020 by Roxy recipes. All rights reserved

  • ooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooroxyrecipes Instagram Account
bottom of page