Supu ya kuku
- Rukhsana Noor
- Jul 7, 2020
- 1 min read
Mahitaji:
Vipande vya kuku unavyotaka
Hoho moja
Carrot moja
Vitunguu maji vitatu
Chumvi
Limao au ndimu moja
Tangawizi iliyopondwa 1/2 tbsp (kijiko cha chakula)
Pilipili manga ya unga 1tsp (kijiko cha chai)
Jinsi ya kupika:
1) Osha vipande vya kuku weka katika sufuria weka chumvi na kamulia ndimu au limao kisha bandika jikoni ichemke iive na ibaki na maji ya kutosha kwa supu kisha epua
2) Toa vipande vya kuku katika supu uliyochemshia weka pembeni, kisha Katakata vitunguu, hoho na carrots weka katika supu uliyochemshia kuku, weka na tangawizi na pilipili manga rudisha jikoni chemsha viive kisha epua ipoe
3) Ikishapoa mimina katika jagi la blender kisha saga ukimaliza mimina ndani ya sufuria weka na vipande vya kuku rudisha tena jikoni kwa dk 2 ichemke kisha epua itakuwa tayari.
Comments