top of page
Search
  • Writer: Rukhsana Noor
    Rukhsana Noor
  • Jul 4, 2020
  • 1 min read


MAHITAJI:


unga wa ngano vikombe viwili (500ml)

Tui la Nazi kikombe kimoja (250ml)

Sukari kikombe kimoja (250ml)

Amira ya chenga 2tbsp

Banking powder 1tsp (mimi hutumia chapa mandashi)

Hiliki ya unga 1tbsp

Chumvi 1/2 tsp

Mafuta ya kupikia


JINSI YA KUPIKA:


1) Chukuwa unga weka katika bakuli pana kisha weka sukari,chumvi, hiliki, mafuta ya kula kijiko kimoja, banking powder changanya weka pembeni , pasha tui liwe vuguvugu chota vijiko vitatu weka katika bakuli dogo weka amira changanya na tui funika iumuke, ikishaumuka mimina katika bakuli la unga changanya kisha tumia tui kukanda unga, kanda mpaka ulainike kisha pakaa donge lako mafuta funika kwa masaa mawili liumuke


2) Likisha umuka kata madonge ya size unayotaka ya mandazi kisha funika tena madonge yaumuke, yakiumuka sukuma donge moja usifanye nene wala jembamba ukisha sukuma kama chapati kata vipande vinne vya mandazi kisha fanya hivyo mpaka madonge yaishe na funika tena mandazi yaumuke yakisha umuka weka karai jikoni tumia moto mdogo mafuta yakipata moto kiasi anza kuchoma mandazi yako mpaka yaishe.

 
 
 
  • Writer: Rukhsana Noor
    Rukhsana Noor
  • May 12, 2020
  • 1 min read

Vanilla cake


MAHITAJI:

unga wa ngano gram 560

Mayai 6

Sukari nusu kilo

Vanilla sugar kijiko kimoja au vanilla ya maji vijiko viwili

Chumvi kijiko kimoja kidogo

Banking soda kijiko kimoja kidogo

Blue band gram 350

Maziwa 310ml


JINSI YA KUPIKA:


1) Weka sukari yote na siagi yote katika bakuli pana na utumie hand mixer kumix mpaka vilainike kavisa viwe laini


2) Kisha weka yai moja moja huku ukiendelea kusaga mpaka yasagike yote na yachanganyike vizuri


3) Kisha anza kuweka maziwa kidogo kidogo huku ukiendeea kumix kisha weka vanilla endelea kumix


4) Kisha anza kuweka unga kidogo kidogo huku unachanganya unaweza tumia mwiko kuchanganyia unga hand mixer haina haja tena ukimaliza andaa kifaa chako cha kuokea kipake mafuta au siagi kisha mimina mcganganyiko wako na uoke keki yako kwa dk45 kwa moto wa 150c, baada ya hapo itakuwa tayari. Enjoy 😋

 
 
 
  • Writer: Rukhsana Noor
    Rukhsana Noor
  • May 12, 2020
  • 1 min read


MAHITAJI:

Unga wa ngano vikombe vitano (tumia 250ml cup)

Siagi iliyoyeyushwa vijiko vikubwa vya chakula viwili

Siagi usiyoyeyusha vijiko vitatu vikubwa vya chakula

Maziwa ya maji nusu lita

Mdalasini wa unga vijiko vitatu vya na nusu vya chakula

Sukari ya brown vijiko vitatu vikubwa

Sukari nyeupe vijiko vitatu vya chakula

Hamira ya chenga kijiko kimoja kikubwa na nusu

Yai moja

Banking powder kijiko kimoja kidogo


JINSI YA KUTENGENEZA:


1) chukuwa bakuli pana weka unga, banking powder na sukari nyeupe changanya weka pembeni


2) Chukuwa bakuli lingine weka sukari ya brown na mdalasini changanya kisha weka pembeni


3) Chukuwa bakuli lingine weka siagi yote iliyoyeyushwa, maziwa, yai na amira ya chenga changanya mpaka amira iyeyuke na ipande juu


4) Kisha tumia mchanganyiko wa maziwa, amira,yai na siagi kuukandia unga kanda unga uwe laini utaona unaganda mikononi ni sawa unaweza pakaa mafuta katika mikono ili usikunatie ukimaliza kukanda unga uweke katika bakuli kubwa lipakae mafuta ili usinatie kisha funika kwa lisaa limoja uumuke


5) ukisha umuka kata madonge ya size kiasi usukume kama chapati donge moja moja


6) Ukisha sukuma donge la kwanza chukuwa siagi isiyoyeyushwa pakaa juu ya hilo donge ulilosukuma hakikisha umepakaa kote kisha chukuwa mchanganyiko wa mdalasini na sukari anza kunyunyizia Juu ukimaliza roll hilo donge lako kisha chukuwa kisu anza kukata madonge unayotaka, fanya hivyo mpaka madonge yako yaishe


7) Chukuwa pan la oven la kuokea pakaa mafuta kisha panga rolls zako acha nafasi kati ya roll moja na nyingine ili ukiumua tena zipate nafasi kisha funika acha tena yaumuke kwa dk 30 yakisha umuka oka katika moto wa 180C kwa dk 25 baada ya hapo toa zitakuwa tayari. Enjoy

 
 
 

© 2020 by Roxy recipes. All rights reserved

  • ooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooroxyrecipes Instagram Account
bottom of page